• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
Katavi Regional Website
Katavi Regional Website

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Tovuti ya Mkoa wa Katavi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Maono na Dhamira
  • Huduma
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na bRasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Halmashauri
      • Miundombinu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • maji
      • Afya
      • Elimu
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Idara ya Fedha na Uhasibu
      • Manunuzi
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
    • Muundo wa Taasisi
  • Machapisho
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Videos
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
  • Wilaya
    • Mpanda
    • Mlele
    • Tanganyika
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Livestock
    • Industry and Fishing
    • Minerals
    • Fishing
  • Utalii
    • Katavi National Park
    • Nkondwe Waterfalls
  • Biashara

Wiki ya Mwanakatavi sasa kuadhimishwa kila Mwaka,RC Katavi awataka Viongozi na Wadau kujipanga.

Posted on: November 2nd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Bi.Mwanamvua Mrindoko amewaelekeza viongozi Mkoani humo kuratibu maadhimisho ya Wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii kila Mwaka ili kutoa fursa kwa Wananchi kujifunza Teknolojia mbalimbali za kisasa pamoja na fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya Kilimo na Utalii,pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya Kilimo na Utalii kutanua wigo wa masoko ya bidhaa zao.

Bi.Mrindoko ameyaasema hayo 2 Novemba 2022 katika kilele cha maadhimisho ya Wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii yaliyopambwa na maonyesho ya bidhaa mbalimbali za Kilimo pamoja na Utalii yaliyodumu kwa muda wa siku 5 katika Uwanja wa Shule ya Msingi Kashato Manispaa ya Mpanda.

Amesema hatua ya kufanya maadhimisho ya Wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii kila mwaka itasaidia kwa sehemu kubwa Mkoa wa Katavi kuongeza uzalishaji wa mazao mbalimbali pamoja na kuleta hamasa ya matumizi ya Teknolojia ya kisasa katika Kilimo na Ufugaji

Aidha Mkuu wa Mkoa Mrindoko amewaelekeza pia Viongozi Mkoani humu wakiwemo Wakuu wa Wilaya pamoja na Wakurugenzi kukamilisha Ujenzi wa Uwanja wa Nanenane ulioanza kujengwa katika eneo la Kabungu Wilaya ya Tanganyika ili kutoa fursa kwa Maonyesho ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii kufanyika katika eneo hilo 

Katika hatua nyingine Bi.Mrindoko amewashukuru viongozi na wadau mbalimbali Mkoani humo kwa waliofanikisha kuratibu maadhimisho ya wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii ambapo pia amewapongeza Wananchi kwa muitikio mkubwa waliouonyesha kushiriki katika Maadhimisho hayo.

Maadhiisho ya Wiki ya Mwanakatavi ya Kilimo na Utalii yamehitimishwa leo baada ya kudumu kwa siku tano tangu kuzinduliwa kwake 28 Oktoba 2022 ambapo shughuli mbalimbali zilifanyika ikiwemo kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii ndani ya Mkoa,uzinduzi wa Filamu ya the Royal Tour,Shindano la kumsaka Mlimbwende wa Utalii Katavi,pamoja na uzinduzi wa Msimu wa Kilimo 2022.

Zaidi ya washiriki 48 zikiwemo Taasisi mbalimbali za Serikali na Mashirika yasiyo ya Kiserikali,Makampuni mbalimbali ya utoaji huduma pamoja na Wajasiriamali wadogo wameshiriki kikamilifu katika maonyesho hayo.


Matangazo

  • No records found
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Katavi aongoza Wananchi kupanda Miti,ahimiza utunzaji wa mazingira,vyanzo vya Maji,akemea vikali shughulli za kibinadamu katika vyanzo vya Maji.

    January 26, 2023
  • RC Kataci aongoza Wananchi kupanda Miti,Ahimiza utunzaji wa mazingira,vyanzo vya Maji,akemea vikali shughulli za kibinadamu katika vyanzo vya Maji.

    January 26, 2023
  • RC Katavi akabidhi pikipiki 8 kwa Maafisa Tarafa. Awataka kutumia vyombo hivyo kufuatilia Ugawaji wa Mbolea,Uripoti wa Wanafunzi Mashuleni.

    January 13, 2023
  • KATAVI WATEKELEZA MAAGIZO YA WAZIRI MKUU, KITUO CHA AFYA MAJIMOTO CHAANZA KUTOA HUDUMA,

    December 30, 2022
  • Tazama Zote

Video

UZINDUZI RATIBA YA SAFARI ZA NDEGE ATCL SIKU YA JUMATATU 23 MEI 2022
Video zinginezo

Wavuti wa Haraka

  • SALARY SLIP PORTAL
  • MWENGE BLOG-KATAVI
  • FURSA ZA UTALII KATUMA MKOANI KATAVI

Wavuti mwambata

  • Mpanda Municipal Council
  • Mpimbwe District Council
  • Mpanda District Council
  • Nsimbo District Council
  • Mlele District Council
  • Tovuti ya utumishi

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

click here

Ramani

Wasiliana nasi

    Mpanda-Katavi (Mkoani Area)

    Sanduku la Barua: Box 235, Mpanda -Katavi

    simu: 025-2957108

    Mobile:

    Barua pepe: ras.katavi@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • ramani
    • Huduma

Copyright@2017 Katavi Rs. All right reserved